Kwa nini iPAB
Hatuuzi software. Tunatengeneza biashara.
Kampuni nyingi za “mifumo” zinakuuzia app halafu zinatoweka. iPAB ilianza kwa kukaa ndani ya biashara za Tanzania; kuhesabu stoo, kuona mauzo yakipotea mlangoni; na kujenga hasa kile kinachozuia hasara. Leo biashara 1,220+ zinatumia iPAB kila siku, kuanzia maduka ya dawa Dar mpaka vyuo vya NACTVET.
“Hatutengenezi app, tovuti, wala mifumo. Tunatatua changamoto za biashara kwa teknolojia.”
— iPAB International Limited
Misingi tunayojishikilia nayo
- 01
Matokeo kuliko vipengele
- 02
Tunafundisha watu, si kufunga mfumo tu
- 03
24/7 maana yake ni 24/7
- 04
Imejengwa Tanzania, kwa uhalisia wa biashara za Tanzania
Watu wanaopokea simu saa nane usiku
Picha ya mwanzilishi + wasifuTODO; italetwa baadaye
Picha ya timuTODO; italetwa baadaye
Tupo Dar es Salaam; tunahudumia biashara Tanzania nzima
Jumatatu–Jumamosi 8:00–17:00
Jua biashara yako inavuja wapi.
Ujumbe mmoja wa WhatsApp. Tutakuambia hasa tungerekebisha nini.